
Miss Tanzania 2006/07 ambaye sasa amejikita kwenye uigizaji wa filamu, Wema Sepetu hivi karibuni alijikuta akilianika kalio lake alipokuwa mjini Morogoro.
Tukio hilo la aibu lilijiri wakati mrembo huyo alipopanda jukwaani kumpa kampani laazizi wake, Naseeb Abdul ‘Diamond’ alipokuwa akipafomu kwenye Tamasha la Fiesta lililofanyika ndani ya Uwanja wa Jamhuri.
Wema ambaye alikuwa amevalia kigauni kifupi, awali alionekana akipanda jukwaani kuimba na Diamond wimbo wa Nitarejea lakini wakati akicheza, kigauni chake kilipanda juu hivyo kuianika sehemu hiyo nyeti.

Kitendo hicho kiliwafanya baadhi ya mashabiki kumzomea huku mwenyewe akidhani walikuwa wakimshangilia.
Aidha, baadhi ya watu waliozungumza na Ijumaa uwanjani hapo walimlaumu Diamond kumpandisha mpenzi wake huyo jukwaani akiwa nusu uchi.

Hata hivyo, katika kuonesha kutojali, wawili hao walinaswa nyuma ya steji .wakipongezana kama walichokifanya ni chamsingi.
No comments:
Post a Comment