
STAA katika tasnia ya filamu Bongo, Yvonne Cherry Ngatikwa ‘Monalisa’, Julai 6, mwaka huu ndani ya Viwanja vya Sabasaba, Mtoni jijini Dar es Salaam alitimua mbio kumkimbia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete.
Monalisa alikuwa kama mtu aliyepandwa na malaria ya ghafla kichwani pale alipomuona ‘laivu’ Rais Kikwete alipokuwa akitembelea mabanda katika viwanja hivyo.
Monalisa akiwa na mama yake, Suzan Lewis ‘Natasha’ pamoja na wasanii wengine waliokuwa kwenye banda la Dk. Rahabu, alitimua mbio baada ya kumuona Rais Kikwete akiwa anatokea mbele yao, akiwa na wapambe wake.

Monalisa pia alisema kuwa rais anatisha kutokana na dola inayomzunguka kiasi cha kufanya watu kutishika na kudhani kuwa siyo mtu wa kawaida.
Baadhi ya watu waliokuwepo eneo hilo waliangua vicheko lakini wengine walimuonea huruma kwa jinsi alivyokosa amani na kukimbia.
No comments:
Post a Comment