Wednesday, July 13, 2011

Penzi la H. Baba



PENZI la mastaa wawili wanaotamba katika tasnia za filamu na muziki Bongo, Hamis Ramadhani Baba ‘H Baba’ na Frola Mvungi limeanza kuchokonolewa na kudaiwa kufanyiwa mambo  ya kishirikina, Risasi Mchanganyiko lina taarifa.

Akizungumza na gazeti hili Jumapili iliyopita katika Viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam, H Baba alisema kuwa, amekumbana na mambo mengi katika uhusiano wake na diva huyo wa filamu.

H Baba.
“Kuna mambo mengi sana nyuma ya pazia ambayo watu hawayajui na kama nisingekuwa mvumilivu ningekuwa nimeshaachana na Flora, “ alisema H Baba.

Mwanamuziki huyo wa Bongo Fleva ambaye pia huigiza filamu, alitoboa kuwa kuna watu wamefikia kuwaendea kwa waganga ili kulivunja penzi lao lakini wanagonga mwamba.

“Yaani kila siku watu wanatutafuta, wengine nawajua kabisa kwa majina, wanajaribu hata kwenda kwa babu ili watuharibie kitu ambacho naamini watajihangaisha bure, mimi namwamini Mungu,” alisema H Baba.
Boniface Ambani.
Mbali ni hilo, H Baba alisema kuwa, mara kadhaa amekuwa akikuta meseji  katika simu ya mpenzi wake huyo kutoka kwa mshambuliaji wa zamani wa Yanga, Boniface Ambani.

“Ambani bado anamsumbua Frola kwani amekuwa akimpigia simu na hata kumtumia SMS  za kumshawishi kimapenzi lakini mimi ninanyamaza kimya tu,” alisema.

Waandishi wetu walipomuuliza H Baba kwamba ni lini wanatarajia kufunga ndoa na Flora, alisema kuwa kwa sasa bado hawajafikia hatua hiyo.

“Bado naendelea kumchunguza, siwezi kumuoa leo wala kesho, unajua  mnaweza kukurupuka kuoana kisha

No comments:

Post a Comment